Na Baraka Mbolembole
STEVEN Mapunda ‘Garrincha’ na Said Maulid ‘SMG’ ni wings wa kwanza wa ‘kizazi cha miaka ya 2000’ ambao walitikisa sana Tanzania kutokana na uchezaji wao wa kasi wakitokea upande wa kulia mwa uwanja. Ma-wings hawa wanabaki kuwa bora kihistoria kwa maana tayari wameshastaafu soka la ushindani.
Mapunda na SMG ni kati ya wachezaji wa kizazi kipya ambao
walikuwa wakicheza kizamani-kwa maana ya kubaki tu sehemu ya pembeni ya
uwanja na kutegemea kukimbia na mpira au kukimbia pasi iliyo ‘njiani.’
Wakati fulani, Saimon Msuva alionekana kama anaweza kuwa ‘Steven
Mapunda mpya’ lakini mifumo ya uchezaji imemzua, huku pia akiwa si
mpigani mzuri wa krosi. Sifa nyingine muhumu ambayo iliwafanya Garrincha
na SMG kutamba ni upigaji wa krosi timilifu ambazo zilifika kwa
walengwa.Pengine ‘uhaba’ wa washambulibji wenye uwezo wa kucheza mipira ya juu ndio umechangia kwa kiasi kikubwa kumepunguza ma-wing wenye ‘krosi bomba,’ ama inawezekana mbinu za makocha wa kisasa, mifumo ya kiuchezaji ama ni kupungua kwa wachezaji namba 7 au 11 wenye maarifa binafsi yenye kuzalisha magoli mengi kwa timu yake.
Hakika hiki si kizazi cha David Beckham wala Sergio Conceicao, hizi si nyakati za wakufunzi kama John Simkoko ndiyo maana wachezaji kama Paul Pogba na makocha kama Mexime wanatawala.
Kama ningekuwa kocha ningependelea mfumo wa 4-4-2 ambao ni rahisi kwa wachezaji wa England ama hapa Tanzania.
Mfumo huu usingempa, Msuva tuzo binafsi za ufungaji bora na
mchezaji bora wa ligi kuu Tanzania Bara msimu wa 2014/15, lakini
unaweza kumpa magoli zaidi ya 30 Zlatan Ibrahimovic pale England. Licha
kuwa ni kibabu, Ibrahimovic angefunga kwa ustadi mkubwa magoli matatu
katika krosi tano za David Beckham.
Rooney alifunga magoli 27 katika EPL msimu wa 2009/10 huku ustadi
wake kuruka juu na kufunga kwa kichwa ukichagizwa na krosi maridadi na
timilifu kutoka kwa Antonio Valencia.Si Alex Ferguson hakuwa na vikosi vikali lakini alikuwa na ‘mbinu za kichawi.’ 4-4-2 imempatia heshima ya miaka yote katika soka la Kingereza kama ambavyo makocha wengi wanavyoangaika kuvunja rekodi ya Simkoko pale Mtibwa Sugar.
Nisingependelea kabisa kuichezesha timu yoyote ya Tanzania
mfumo wa 4-3-3, na kama ningekuwa mshauri wa Jose Mourinho ningemshauri
aachane na mbinu zote na kwa kuwa nafahamu ubora wake wa kimbinu
ningemwambia ‘a-copy na ku-paste’ 4-4-2 ya Sir Alex. Rooney ni namba 10
bora zaidi England na Valencia si namba 2 na wing bora zaidi wa kulia
pale England.
Unawakumbuka, Abuu Mkangwa, Geofrey Mhando, Moja Liseki,
Abdallah Juma-Mzanzibar pekee kushinda tuzo ya ufungaji bora VPL. Hao
niliokutajia hapo wote wamefanya mambo makubwa pale Mtibwa na wameshinda
tuzo za ufungaji bora VPL wakiwa pale.